Katika kilele cha Maadhimisho ya wiki ya huduma kwa Jamii,Mh.Diwani wa kata ya Bigwa Bw.Richard Mmanda amezinduwa huduma ya matengenezo ya vyombo vya moto(Garage) katika karakana ya ufundi wa magari Chuoni na pia aliwaomba wananchi kuunga mkono juhudi za chuo kwa kuleta vyombo vyao vya usafiri kwaajili ya matengenezo
Mkuu wa Chuo Bi.Monica Lukeha Ametoa sukrani za dhati kwa jamii pia alisema Uwepo wa huduma ya gereji utasaidia wanafunzi katika kujifunza kwa vitendo na kuyafanya mafunzo kuwa na ufanisi.